Coat of Arms

PUBLIC SERVICE SOCIAL SECURITY FUND

Leo. Kesho. Pamoja.

PSSSF Logo
PSSSF yawanoa Jeshi la Polisi Tanzania jinsi ya kuwasilisha nyaraka kidijitali

PSSSF yawanoa Jeshi la Polisi Tanzania jinsi ya kuwasilisha nyaraka kidijitali

Operations Director
#Kidigitali #Meetings

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Utumishi wa Umma (PSSSF) umeendesha mafunzo ya namna ya kuwasilisha madai kupitia mifumo ya ICT kwa maafisa wa Dawati la Mafao wa Jeshi la Polisi Tanzania.

Akizungumza katika hotuba ya ufunguzi kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi, Tanzania IGP Carmilius Wambura, CP Suzanne Kaganda alisema mfumo wa kuwasilisha nyaraka utasaidia wanachama kufuatilia madai yao wenyewe kwa haraka na uwazi. "Ninawahimiza kutumia fursa hii ya kipekee, kuwa wepesi kujifunza ili muweze kwenda na kasi ya teknolojia."


Akitoa salamu kwa niaba ya PSSSF, Mkurugenzi Mkuu, Bwana Abdul-Razaq Badru alisema PSSSF imetehemisha operesheni zake ili kuboresha huduma kwa wanachama na wadau. "Jeshi la Polisi ni moja ya makundi maalum yanayohudumiwa na PSSSF kwa kutumia huduma zetu za kidijitali, tunajitahidi kutoa huduma sahihi na kuondoa mnyororo wa utoaji huduma."