• Call Free: 0800 110040
  • Portal Admin Form
 
  • Change Language: SW
 
  • Enquiries
  • FAQs
  • Home
  • About PSSSF
    • About Us
    • Organisation Offices
    • Board of Trustees
    • Management
  • Benefits
    • Retirement Benefit
    • Death Benefit
    • Survivor Benefit
    • Maternity Benefit
    • Unemployment Benefit
    • Sickness Benefit
    • Invalidity Benefit
  • Media Center
    • News
    • Publications
    • Photo Album
    • Video
  • Self Service
    • Member Portal
    • Billing Portal
    • QR-Codes
    • Portal Admin Form
  • Investments
    • Real Estate
    • Industial Investment
  • Tenders
    • General Procurement Notice
    • Awarded
    • Current Tender
  • e- Mrejesho
 
  Home   |   News Board
author image

PSSSF

To provide high quality social security services using competent, motivated staff and appropriate technology.

Benefit Types

  • Retirement Benefit
  • Death Benefit
  • Survivour Benefit
  • Maternity Benefit
  • Unemployment Benefit
  • Sickness Benefit
  • Invalidy Benefit

Online Services

  • Member Portal
  • Billing Portal
  • QR-Codes
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF Ahudhuria Maadhimisho ya Wiki ya Tume ya Utumishi wa Umma
2024-09-29 00:00:00

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw. Paul Kijazi, akipokea cheti cha kutambua mchango wa Mfuko kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma, Jaji Mstaafu Hamisa Hamisi Kalombola, wakati wa maadhimisho ya kilele cha wiki ya Tume ya Utumishi wa Umma jijini Dodoma.

*Aahidi Ushirikiano na Kuboresha Huduma Kidijitali

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw. Paul Kijazi, audhuria kilele cha maadhimisho ya wiki ya Tume ya Utumishi wa Umma tarehe 29 Septemba, 2024, jijini Dodoma, alitoa pongezi kwa Tume kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuboresha masuala ya utumishi wa umma. Aliahidi ushirikiano wa karibu kati ya PSSSF na Tume hiyo ili kuhakikisha watumishi wa umma wanapata haki zao kikamilifu, huku akisisitiza umuhimu wa taasisi hizo mbili kufanya kazi kwa pamoja.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw. Paul Kijazi, akizungumza wakati wa maadhimisho ya kilele cha wiki ya Tume ya Utumishi wa Umma jijini Dodoma,

Bw. Kijazi pia alielezea juhudi za PSSSF katika kuboresha huduma kwa wanachama wake kupitia matumizi ya teknolojia ya kidijitali. Alifafanua kwamba Mfuko umefanikiwa kusogeza karibu huduma kwa wanachama kwa njia ya kidijitali, hatua ambayo imeongeza ufanisi na kupunguza usumbufu Wanachama na Wastaafu.

“Sasa wanachama wanaweza kufuatilia michango yao, kuwasilisha maombi, na kupata taarifa zote muhimu kupitia simu au kompyuta zao bila kulazimika kufika ofisini. Hii imesaidia sana kupunguza muda wa kusubiri na kurahisisha upatikanaji wa huduma,” alisema Bw. Kijazi.

Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Mathew Modest Kilama, akizungumza wakati wa maadhimisho ya kilele cha wiki ya Tume hiyo jijini Dodoma, kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Jaji Mstaafu Hamisa Hamisi Kalombola. Bw. Kilama alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za umma ili kuboresha utendaji na utoaji wa huduma kwa watumishi wa umma.

Alibainisha pia kuwa Mfuko umewekeza katika kuboresha miundombinu ya usalama wa taarifa za wanachama ili kuhakikisha kuwa faragha na usalama wa taarifa zao zinalindwa kwa kiwango cha juu zaidi. “Tunataka wanachama wetu wawe na amani ya akili wanapotumia huduma zetu za kidijitali, wakijua kuwa taarifa zao ziko salama.”

Kwa kumalizia, Bw. Kijazi alisisitiza kuwa mapinduzi ya kidijitali ndani ya PSSSF yanalenga kuboresha zaidi huduma kwa wanachama na kwamba ushirikiano kati ya PSSSF na Tume ya Utumishi wa Umma utaimarishwa zaidi ili kuleta matokeo chanya kwa watumishi wa umma.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw. Paul Kijazi, akizungumza na wadau mbalimbali wakati wa hafla ya maadhimisho ya kilele cha wiki ya Tume ya Utumishi wa Umma jijini Dodoma

About PSSSF

The main purpose is to collect contributions and payment of terminal benefits to employees of public service.The act shall apply in mainland Tanzania.


READ MORE

Quick Links

  • Billing Portal
  • Member Portal
  • Employer Portal
  • Announced Tenders

Get In touch

  • PSSSF House HQ , Makole, Dodoma
  • P.O.BOX 1501
  • info@psssf.go.tz
  • 0800 110040
  • Mon - Fri 8.00 - 17.00. Sat,Sun CLOSED

Zonal Offices

  • Dodoma: +255 26 2323338
  • Ilala: +255 22 2120912
  • Kinondoni: +255 22 2123848
  • Temeke: +255 22 2861039
  • Mwanza: +255 28 2506114
  • Mbeya: +255 25 2502243
  • Arusha: +255 27 2970284
  • Morogoro: +255 23 2934188
  • Mtwara: +255 23 2334661
  • Geita: +255 28 2520470
Copyright © 2024 psssf. All rights reserved.
  • Contact Us
  • Privacy Policy
  • Services
  • Disclaimer