SAUTI ZA WANACHAMA
Benefits
#Kidigitali
#Meetings
#Pension
Aidha, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Augustine Vumma Hole, alishauri kiwanda hicho kuboresha bidhaa wanazozalisha kuendana na wakati bila kuacha ubora. "Jitahidini sana mnyumbulike kwenye fasheni bila kuacha ubora unaotakiwa kitaifa na kimataifa, mpaka sasa mmefanya kazi nzuri." Alisema Mhe. Vuma.
Mhe. Vuma, pia alipongeza uzalishaji unaofanyika katika kiwanda hicho pia kuongeza uzalishaji ili kuhakikisha fedha zilizowekwa na Serikali katika mradi huu zirudi kwa wakati. Wajumbe wa Kamati hiyo walishauri kutafuta kampuni makubwa ya uzalishaji bidhaa za ngozi ili kushirikiana nao.